HISTORIA YA PAROKIA YA KRISTU MCHUNGAJI MWEMA – BUZURUGA

Kuanzishwa kwa Kigango na Parokia

Kigango cha Buzuruga kilizaliwa kutoka Parokia ya Nyakato tarehe 13/10/1992. Mnamo tarehe 26/10/2004, Mheshimiwa Baba Askofu Mkuu alitangaza rasmi Kigango cha Buzuruga kuwa Parokia Teule. Parokia hii ilizinduliwa rasmi kuwa Parokia kamili na Mheshimiwa Baba Askofu Mkuu Hayati Anthony Petro Mayala tarehe 26/11/2006, ikiwa na vigango vitatu: Nyasaka, Bugarika (Mwananchi) na Buzuruga.

Upatikanaji wa Eneo

Eneo la Parokia ya Buzuruga lilinunuliwa kutoka kwa Mzee Ally Jumanne mwaka 1992 kwa kiasi cha Tsh. 100,000 (Laki moja tu). Lina ukubwa wa hekta 2.5 na limepimwa rasmi na kutolewa hati miliki Plot No. 964 Kitalu HH Nyakato.

Viongozi Waanzilishi wa Parokia

Mapadre wa Kwanza:

  • Padre Antony Sami – CMF (2004 – 2006)

Viongozi wa Halmashauri ya Walei:

  1. Innocent Walwa – Mwenyekiti

  2. Justius Mwita – Makamu Mwenyekiti

  3. John Chonja – Katibu

  4. Cyriacus Lweyendeza – Katibu Msaidizi

  5. Mercia Mondea – Mhasibu

Jiografia ya Parokia

  • Ukubwa wa eneo: Hekta 2.5, linalozungukwa na milima upande wa Kaskazini na barabara iendayo Nyambiti.

  • Idadi ya Jumuiya: 30

  • Idadi ya Mitaa/Kanda: 4 (A, B, C na D)

  • Parokia hii haina vigango, bali ina Kanda nne zinazoiunda.

  • Makadirio ya idadi ya waamini: 1,500

Vyama vya Kitume

  • Uwaka

  • Wawata

  • Viwawa

  • Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu

Vyama vya Karama

  • Watumikiaji

  • Moyo Mtakatifu wa Yesu

  • Rozari Hai

  • Radio Maria

  • Karesmatiki Katoliki

  • Kwaya ya Kristo Mchungaji Mwema

  • Kwaya ya Yohana Paulo wa II

Kamati za Idara katika Parokia

  • Kamati ya Kiuchungaji

  • Kamati ya Liturujia

  • Kamati ya Elimu

  • Kamati ya Mawasiliano

  • Kamati ya Sherehe

  • Kamati ya Ardhi na Mazingira

  • Kamati ya Familia

  • Kamati ya Karitas

  • Kamati ya Utume wa Walei

  • Kamati ya Afya

  • Kamati ya Katekesi

  • Kamati ya Ulinzi

Taasisi Zilizopo

  • Mnara wa Vodacom (sasa inamilikiwa na Tigo)

Orodha ya Maparoko Waliohudumu

MwakaParokoParoko Msaidizi
2004 – 2006Fr. Anthony Sami-
2006 – 2010Fr. Jesuraj MichaelKulandey Sami
2009-Fr. Stephen Arulsamy
2010-Fr. John Britto
2010 – 2012Fr. Stephen ArulsamyFr. John Britto
2012Fr. William Baskar-
2012Fr. Abel MwarabuFr. John Britto, Fr. William Baskar
2014Fr. Abel MwarabuFr. Thadeus Mchomba, Fr. John Britto
2016Fr. Abel MwarabuFr. Jonas Chellappan
2017Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. Jonas Chellappan
2017Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. Emmanuel Vethamuthu, Fr. Gabriel Bolan
2019Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. Midhun Pullickal
2020Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. John Britto
2021Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. John Britto, Rev. Bazilio Kyaligonza
2022 (Julai)Fr. Chukwuemeka AnyanwuFr. Bazilio Kyaligonza
2022 (Oktoba)Fr. Pius NwankwoFr. Bazilio Kyaligonza
2023Fr. Pius NwankwoFr. John Obonyo
2024Fr. Pius NwankwoFr. John Obonyo

Miradi ya Parokia

  • Ujenzi wa Kanisa (mpango wa upanuzi)

  • Ukumbi wa Matumizi Mbalimbali (tayari unatumika)

Vyanzo vya Mapato

  • Sadaka

  • Zaka

  • Harambee ya kila mwisho wa mwezi (maarufu kama Harambee ya Bluu)

  • Michango ya Jumuiya

  • Ukodishaji wa ukumbi

  • Wafadhili wa ndani ya Parokia

Huduma za Kiroho

  • Misa Takatifu

  • Sakramenti: Ubatizo, Komunio, Kipaimara, Kitubio, Ndoa

  • Kutembelea wagonjwa na kuwapa mpako wa wagonjwa

  • Mapadre wanatembelea waamini kwenye Jumuiya kwa ajili ya kuwaimarisha kiroho

Miito ya Kipadre

  • Mapadre waliotoka Parokia ya Buzuruga:

    1. Felician Nuru

    2. Steven Bikolwamungu

  • Waseminari: Watatu wanaendelea na wito wao

  • Idadi ya Makatekista: Wawili

Parokia Jirani

  • Kaskazini: Parokia ya Nyasaka

  • Mashariki: Parokia ya Nundu

  • Kusini: Parokia ya Mwananchi

  • Magharibi: Parokia ya Mabatini

Shughuli za Waamini

  • Wafanyakazi

  • Wafanyabiashara

  • Wajasiriamali

  • Wastaafu

Mafanikio

  • Ujenzi wa ukumbi

  • Ujenzi wa uzio kuzunguka Parokia

  • Ujenzi wa kanisa dogo la kuabudia

  • Ununuzi wa Generator kubwa

  • Mchango wa kila mwaka kwa Jimbo

Changamoto

  • Kuhama kwa waumini kutokana na uhaba wa viwanja

  • Mahudhurio hafifu kwenye vikao na Jumuiya

  • Changamoto ya barabara mbovu inayopunguza wateja wa ukumbi

Malengo ya Baadaye

  • Upanuzi wa Kanisa

  • Ujenzi wa Chekechea

  • Kuimarisha Elimu ya Dini Mashuleni

Shukurani

Tunawashukuru wachungaji wetu kwa kutuhudumia kiimani na kiroho. Pia tunawashukuru waamini wote wa Parokia ya Buzuruga kwa kuijenga Parokia yetu.

Orodha ya Jumuiya zinazounda Parokia ya Buzuruga

  1. Mt. Marko
  2. Mt. Batlomeo
  3. Mt. Yuda Thadei
  4. Mt. Dominicko
  5. Mt. Clement
  6. Mt. Mathayo
  7. Mt. Benedicto
  8. Mt. Secilia
  9. Mt. Thomas
  10. Mt. Magdalena
  11. Mt. Flora
  12. Maria Mama wa Mungu
  13. Bikira Maria Mlima Karmeli
  14. Mt. Martha
  15. Epifania
  16. Mt. Fransisco
  17. Mt. Don Bosco
  18. Mt. Raphael
  19. Mt. Pius X
  20. Mt. Ritha
  21. Mt. Alberto
  22. Maria Mama wa Yesu
  23. Mt. Gabriel
  24. Mt. Yosefu
  25. Mt. Paulo
  26. Mt. Michael
  27. Mt. Stephano
  28. Mt. Petro
  29. Mt. Yohana Mbatizaji
  30. Mt. Klareti