• archmwanza@gmail.com
  • +255 769 523 036

Parokia ya Bujora

Parish Details

Kanisa la Mt. Cecilia BUJORA

Najua umewahi kuona makanisa mengi hapa africa ambayo mara zote yamekuwa yakijifananisha na tamaduni za ulaya kutokana na historia ya kanisa ilivyo. Makanisa yote yamekuwa yakijengwa kufananishwa na jinsi makanisa ya KIZUNGU yalivyo na kuitwa majina ya huko yalipoanzia na pia kuwaonesha Yesu na mitume wake kama wazungu n.k 

Sasa, kuna kanisa lipo Bujora Mwanza. Hili ni la kipekee! Lilijengwa na mzungu lakini kini limejengwa kwa kufuata tamaduni za kisukuma. Kuanzia jengo na vitu vilivyomo ndani na hata sanamu ndani ni za sura za kiAfrica pamoja na Yesu mwafrica. Inapendeza sana jinsi ambavyo jamii hii ya wasukuma ilivyofikiwa na hawa wamishionari. Hebu jionee mwenyewe hizi picha za kanisa hilo.

Parish Images

Parish Videos