• archmwanza@gmail.com
  • +255 769 523 036

Parokia ya Sumve

Parish Details

Parokia ya Sumve

Asili ya jina Sumve lilikuwa Busumabu lakini kutokana na utata

wa matamshi kwa wazungu lilifupishwa mwanzoni na kuwa

Sumva kisha likawa Sumve. Mapema mwaka 1897 makatekista

kutoka Bukumbi walitumwa Sumve, Nera, Ngasani na Sumbuka,

ambapo vigango vikajengwa. Mapadre pale Rukumbi wakawa

na shughuli nyingi kiasi kwamba wakashindwa kuvitembealea

vigango hivyo mara kwa mara vikabaki chiral ya uangalizi wa

makatekista.

Kuzinduliwa kwa uinjilishaji Rwanda kulisababisha juhucli na

rasilimali watu vielekezwe zaidi huko. Miaka kumi ya mwanzo

wa karne ya kumi na tisa hapakufanyika juhudi zozote za

uinjilishaji kusini mwa Bukumbi. Pia Askofu Hirth hakuona

umuhimu sana wa kuwekeza maeneo hayo. Mnao mwaka 1910

Padre Bourget na Huguenot walitumwa kutembelea Nera na

Busumabu, wakakuta waprotestanti waliisha jitwalia Nera.

Watawala wa Kikoloni hawakuruhusu mashirika mawili ya dini

yenye ushindani kufanya shughuli zao sehemu moja. Hivyo

Sumve ikachaguliwa kwa unjilishaji mpya. Mwanzoni mapadre

waliishi katika pagale moja kubwa lililokuwa linatumika karna

darasa, lilikuwa wazi bila milango wala madirisha. Usiku walilala

kwa hofu ya kuliwa na fisi au chui. Jitihada za ujenzi wa nyumba

zilianza kwa kuchoma matofali i6o,000. Baada ya mwaka mmoja nyumba kubwa na nzuri ilikamilika. Ikafuatia ujenzi wa Kikanisa cha ukubwa wa mt. 27

Mtemi Kibiti wa Usumao akiwa na umri wa miaka 60, siku za nyuma aliishaalikwa na Askofu Hirth kuhudhuria sherehe za kubariki kanisa la Bukumbi. Yeye alikuwa ni rafiki yake. Hivyo mapadre hawakupata usumbufu. Walivutiwa na moyo wa juhudi na kazi waliokuwa nao wasukuma katika kulima mtama ambao ulikabiliana na hali ya ukame, na kilimo cha mpunga wakati wa masika na mazao ya mahindi, karanga na mhogo. Walikuwa na utajiri wa mifugo, ng’ombe, mbuzi na kondoo. Mifugo yao hapo nyuma ilishambuliwa na ugonjwa wa sotoka ikanusurika kutoweka. Walifika mara kwa mara kwenye zahanati kwa ajili ya huduma za matibabu, lakini shuleni ni wazazi wakristu ndiyo walioruhusu watoto wao kwenda shule licha ya juhudi kubwa na ushawishi uliofanywa na mapadre kwa kuwatembelea majumbani mwao.

Walipinga hayo mafundisho ya imani. Kijana mmoja wa miaka kumi na sita alikamilisha vizuri mafundisho ya ukatekumeni. Kabla ya ubatizo baba yake alimtisha kuwa akibatizwa atakwenda kuishi mbali na nyumbani kwao. Akaacha kuhudhuria Kanisani, lakini akaendelea kusali nyumbani. Kupanuka na kuongezeka kwa ukristu Sumve kutafuatia na kuanza kwa vita ya kwanza ya dunia.

Parish Images

Parish Videos